Acts 10:9-16

Maono Ya Petro

9 aSiku ya pili yake, walipokuwa wameukaribia mji, wakati wa adhuhuri, Petro alipanda juu ya nyumba kuomba. 10 bAlipokuwa akiomba akahisi njaa, akatamani kupata chakula. Lakini wakati walikuwa wakiandaa chakula, akalala usingizi mzito sana. 11 cAkaona mbingu zimefunguka na kitu kama nguo kubwa kikishushwa duniani kwa ncha zake nne. 12Ndani yake walikuwepo aina zote za wanyama wenye miguu minne, nao watambaao nchini, na ndege wa angani. 13Ndipo sauti ikamwambia “Petro, ondoka, uchinje na ule.”

14 dPetro akajibu, “La hasha Bwana! Sijawahi kamwe kula kitu chochote kilicho najisi.”

15 eIle sauti ikasema naye mara ya pili, “Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.”

16Jambo hili lilitokea mara tatu na ghafula ile nguo ikarudishwa mbinguni.

Copyright information for SwhNEN